Italia
Repubblica Italiana (Kiitalia) | |||
![]() |
![]() |
||
Wimbo wa taifa "Il Canto degli Italiani"(Kiitalia) "Wimbo wa Waitalia" |
|||
Eneo la Italia katika bara la Ulaya |
|||
Jiji kubwa (na Mji Mkuu) |
Roma | ||
---|---|---|---|
Lugha rasmi | Kiitalia | ||
Kabila |
|
||
Dini | |||
Utaifa | Miitalia | ||
Aina ya Serikali | Jamhuri ya Muungano wa Rais | ||
Rais | Sergio Mattarella | ||
Waziri Mkuu | Giorgia Meloni | ||
Rais wa Seneti | Ignazio La Russa | ||
Historia | |||
Muungano | 17 Machi 1861 | ||
Jamuhuri | 12 Juni 1946 | ||
Katiba ya sasa | 1 Januari 1948 | ||
Ukubwa wa eneo | |||
Jumla | 301,340 km² | ||
Asilimia ya Maji | 1.24 % | ||
Idadi ya Watu | |||
Mwaka wa Makisio | |||
Idadi ya watu (makisio) | ![]() |
||
Pato la Taifa PPP | |||
Mwaka wa Makisio | 2024 | ||
Jumla | ![]() |
||
Capita | ![]() |
||
Pato la Taifa | |||
Mwaka wa Makisio | 2024 | ||
Jumla | ![]() |
||
Capita | ![]() |
||
Kiashiria cha Maendeleo ya Watu (2022) | ![]() Maendeleo ya Juu Sana |
||
Kiashiria cha ukosefu wa usawa (2021) |
34.8
Ukosefu wa usawa wa kati |
||
Sarafu | Euro € EU | ||
Eneo la saa | UTC+1 (CET) | ||
Nambari ya mwito | +39 | ||
Upande wa Gari | Kulia | ||
Intaneti TLD | .it |
Italia, rasmi Jamhuri ya Italia, ni nchi iliyopo Kusini mwa Ulaya. Inapakana na Ufaransa upande wa magharibi, Uswisi na Austria upande wa kaskazini, na Slovenia upande wa mashariki. Nchi hii ina idadi ya watu takriban milioni 60 na ina eneo la kilomita za mraba 301,340. Roma, jiji kubwa zaidi, pia ni mji mkuu. Italia imegawanywa katika mikoa 20 na inajulikana kwa alama zake za kihistoria, sanaa, vyakula, na kama mahali pa kuzaliwa kwa Dola la Kirumi na Renaissance.
Jiografia
Umbo la jamhuri, kama lile la rasi yake, linafanana na mguu linalozungukwa na maji ya Mediteraneo pande tatu.
Milima ya Appennini inaunda uti wa mgongo wake, wakati ile ya Alpi, ambayo ni mirefu zaidi, inaunda kwa kiasi kikubwa mpaka kati ya Italia na nchi nyingine za Ulaya.
Mlima mrefu zaidi, ukiwa na mita 4,810 juu ya usawa wa bahari, unaitwa Monte Bianco (Mlima Mweupe) na uko mpakani kwa Ufaransa.
Visiwa viwili vikubwa vya Sisilia na Sardinia ni sehemu za Italia pamoja na visiwa vingi vidogovidogo, vile vya Pelagie vikiwa upande wa Afrika.
Italia ina volkeno 14, ambazo 4 kati yake ziko hai: ile ndefu zaidi kuliko zote za Ulaya (mita 3,329) inaitwa Etna na iko mashariki mwa Sisilia. Italia inaongoza Ulaya kwa wingi wa matetemeko ya ardhi.
Mto mrefu zaidi unaitwa Po na una urefu wa kilomita 652. Mito mingine mirefu ni Adige, Tevere, Adda, Oglio, Tanaro, Ticino, Arno, Piave, Reno, Sarca-Mincio n.k.
Maziwa makubwa zaidi ni: Garda (km2 367.94), Ziwa Maggiore (212.51, likiingia Uswisi), Ziwa la Como (145.9), Trasimeno (124.29) na Ziwa la Bolsena (113.55).
Kutokana na urefu mkubwa wa Italia toka kaskazini hadi kusini, hali ya hewa ni tofauti sana, kuanzia baridi kali sana hadi joto kali sana.
Mikoa
Bendera | Jina | Makao makuu | Eneo (km2) | Wakazi | Msongamano wa watu/km² | Wilaya | Miji | Miji mikubwa | Hali ya utawala |
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
![]() |
Abruzzo | L'Aquila | 10,763 | 1,307,919 | 122 | 4 | 305 | - | Kawaida |
![]() |
Bonde la Aosta | Aosta | 3,263 | 126,933 | 39 | 0 | 74 | - | Kujitawala |
![]() |
Puglia | Bari | 19,358 | 4,045,949 | 209 | 6 | 258 | Bari | Kawaida |
![]() |
Basilicata | Potenza | 9,995 | 575,902 | 58 | 2 | 131 | - | Kawaida |
![]() |
Calabria | Catanzaro | 15,081 | 1,954,403 | 130 | 5 | 409 | Reggio Calabria | Kawaida |
![]() |
Campania | Napoli | 13,590 | 5,761,155 | 424 | 5 | 551 | Napoli | Kawaida |
Emilia-Romagna | Bologna | 22,446 | 4,354,450 | 194 | 9 | 348 | Bologna | Kawaida | |
![]() |
Friuli-Venezia Giulia | Trieste | 7,858 | 1,219,356 | 155 | 4 | 218 | Trieste | Kujitawala |
![]() |
Lazio | Rome | 17,236 | 5,550,459 | 322 | 5 | 378 | Rome | Kawaida |
![]() |
Liguria | Genoa | 5,422 | 1,565,349 | 289 | 4 | 235 | Genoa | Kawaida |
![]() |
Lombardia | Milan | 23,861 | 9,749,593 | 409 | 12 | 1544 | Milan | Kawaida |
![]() |
Marche | Ancona | 9,366 | 1,541,692 | 165 | 5 | 239 | - | Kawaida |
![]() |
Molise | Campobasso | 4,438 | 312,394 | 70 | 2 | 136 | - | Kawaida |
![]() |
Piemonte | Turin | 25,402 | 4,366,251 | 172 | 8 | 1206 | Turin | Kawaida |
![]() |
Sardinia | Cagliari | 24,090 | 1,637,193 | 68 | 8 | 377 | Cagliari | Kujitawala |
![]() |
Sisilia | Palermo | 25,711 | 4,994,817 | 194 | 9 | 390 | Catania, Messina, Palermo | Kujitawala |
![]() |
Trentino-Alto Adige/Südtirol | Trento | 13,607 | 1,036,707 | 76 | 2 | 333 | - | Kujitawala |
![]() |
Toscana | Firenze | 22,994 | 3,679,027 | 160 | 10 | 287 | Firenze | Kawaida |
![]() |
Umbria | Perugia | 8,456 | 885,535 | 105 | 2 | 92 | - | Kawaida |
![]() |
Veneto | Venisi | 18,399 | 4,865,380 | 264 | 7 | 581 | Venisi | Kawaida |
Historia
Akiolojia imethibitisha uwepo wa Homo neanderthaliensis miaka 128,000-187,000 hivi iliyopita. Homo sapiens sapiens alifika miaka 40,000 hivi iliyopita.
Kufikia milenia ya 1 KK wakazi wengi walikuwa wa jamii ya Kizungu na kutumia lugha za Kihindi-Kiulaya.
Peninsula ya Italia iliunganishwa mara ya kwanza na Jamhuri ya Roma (509-27 KK), lakini hiyo ilipoenea Ulaya kusini na magharibi, Afrika ya Kaskazini na Asia ya Magharibi ikawa na sura ya kimataifa kama Dola la Roma.
Umoja ulipotea kuanzia uvamizi wa jiji la Roma uliofanywa na Wagermanik (476 BK) na hasa baada ya ufalme wa Karolo Mkuu aliyetawala sehemu ya kaskazini tu.
Juhudi za kuurudisha umoja zilifanywa hasa katika karne ya 19, ambapo Ufalme wa Sardinia uliteka sehemu kubwa ya Italia (hasa miaka 1860, 1866 na 1870) na kubadilika kuwa Ufalme wa Italia wenye makao makuu Roma.
Baada ya vita vikuu vya pili iligeuka Jamhuri yenye katiba inayotia mamlaka kuu mikononi mwa bunge.
Ni kati ya nchi sita zilizoanzisha Umoja wa Ulaya mwaka 1957 ikaendelea kuunga mkono ustawi wake hadi uanzishaji wa pesa ya pamoja (Euro).
Maendeleo
Italia ni kati ya nchi zilizoendelea, ikiwa na nafasi ya nane kwa nguvu ya uchumi duniani, hivyo ni mwanachama wa G7, G8 na G20.
Sanaa na utalii
![](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/7/7e/Collage_chiese_italiane.jpg/250px-Collage_chiese_italiane.jpg)
Italia ndiyo nchi inayongoza duniani kwa kuwa na mahali pengi (51) pa kimaumbile na pa kihistoria palipoingizwa katika orodha ya UNESCO ya "Urithi wa Dunia".
Kwa sababu hiyo pia inashika nafasi ya 5 kati ya nchi zote zilizo lengo la utalii.
Watu
Wananchi wana sifa za pekee kati ya Wazungu wote, hata upande wa DNA, kutokana na jiografia na historia ya rasi.
Ni kati ya nchi ambamo watu wanatarajiwa kuishi miaka mingi zaidi, lakini pia ni kati ya nchi ambapo uzazi ni mdogo zaidi: wanaokufa ni wengi kuliko wanaozaliwa.
Kutokana na umati wa Waitalia waliohama nchi hiyo karne za nyuma, sasa zaidi ya watu milioni 60 nje ya Italia wana asili ya nchi hiyo, mbali na raia zaidi ya milioni 4 wanaoishi nje.
Lugha rasmi ni Kiitalia, inayotegemea zaidi lahaja za Italia ya Kati, lakini siku hizi inatumiwa na wananchi walio wengi hata katika mikoa mingine, ambayo kwa jumla ni 20.
Upande wa dini, wengi wao (81.2%) ni Wakristo wa Kanisa Katoliki, wakifuatwa na Waorthodoksi (2.8%, wengi wao wakiwa wahamiaji, hasa kutoka Romania) na Waprotestanti (1.1%, wengi wao wakiwa Wapentekoste). Uhamiaji mwingi wa miaka ya mwisho wa karne ya 20 umeleta pia Uislamu (3.7%) na dini nyingine.
Dini zote zinaachiwa uhuru na, tofauti na nchi nyingi za Ulaya, waumini wake wanajitahidi kiasi kufuata ibada (29% kila wiki).
Watu maarufu
- Fransisko wa Asizi
- Marko Polo
- Dante Alighieri
- Katerina wa Siena
- Bernardino wa Siena
- Kristofa Columbus
- Amerigo Vespucci
- Yohane wa Verrazzano
- Nikola Machiavelli
- Leonardo wa Vinci
- Michelangelo
- Raffaello Sanzio
- Karolo Borromeo
- Papa Pius V
- Galileo Galilei
- Amedeo Avogadro
- Alessandro Volta
- Giuseppe Verdi
- Giuseppe Garibaldi
- Yohane Bosco
- Antonio Meucci
- Papa Pius X
- Maria Montessori
- Guglielmo Marconi
- Benito Mussolini
- Enrico Fermi
- Papa Yohane XXIII
- Papa Paulo VI
- Pio wa Pietrelcina
- Carlo Rubbia
Tazama pia
Tanbihi
- ↑ 1.0 1.1 1.2 1.3 "Italy GDP profile". Iliwekwa mnamo 2025-01-30.
- ↑ "Italy Hdi". Iliwekwa mnamo 2025-01-31.
- ↑ "The Duomo of Florence | Tripleman". tripleman.com. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2009-12-06. Iliwekwa mnamo 25 Machi 2010.
{cite web}
: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "Brunelleschi's Dome". Brunelleschi's Dome.com. Iliwekwa mnamo 25 Machi 2010.
{cite web}
: CS1 maint: date auto-translated (link) - ↑ "St. Peter's Basilica (Basilica di San Pietro) in Rome, Italy". reidsitaly.com.
- ↑ See List of largest church buildings in the world; note that the #3 entry, First Family Church building in Kansas, is now a school education complex.
- ↑ "Basilica di San Marco". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2015-03-05. Iliwekwa mnamo 10 Februari 2016.
{cite web}
: More than one of|accessdate=
na|access-date=
specified (help)CS1 maint: date auto-translated (link)
Marejeo
- Italy - Eyewitness Travel Guides. DK. 2005. ISBN 1-4053-0781-1.
- Northern Italy - Insight Guides. APA Publications. 2004. ISBN 981-234-903-0.
- Hacken, Richard. "History of Italy: Primary Documents". EuroDocs: Harold B. Lee Library: Brigham Young University. Iliwekwa mnamo 6 Machi 2010.
{cite web}
: CS1 maint: date auto-translated (link) - "FastiOnline: A database of archaeological excavations since the year 2000". International Association of Classical Archaeology (AIAC). 2004–2007. Iliwekwa mnamo 6 Machi 2010.
{cite web}
: CS1 maint: date auto-translated (link) - "Italy History – Italian History Index" (kwa Italian na English). European University Institute, The World Wide Web Virtual Library. 1995–2010. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2021-08-15. Iliwekwa mnamo 6 Machi 2010.
{cite web}
: CS1 maint: date auto-translated (link) CS1 maint: unrecognized language (link)
Viungo vya nje
- Online resources about Italy Ilihifadhiwa 16 Desemba 2008 kwenye Wayback Machine. at UCB Libraries GovPubs
- Italia katika Open Directory Project
- Italian Higher Education for International Students
- Italian National and Regional parks
- Italian tourism official website Ilihifadhiwa 18 Oktoba 2009 kwenye Wayback Machine.
Nchi za Umoja wa Ulaya | ![]() |
---|---|
Austria | Bulgaria | Eire | Estonia | Hispania | Hungaria | Italia | Kroatia | Kupro | Latvia | Lituanya | Luxemburg | Malta | Polandi | Slovakia | Slovenia | Romania | Ubelgiji | Ucheki | Udeni | Ufaransa | Ufini | Ugiriki | Uholanzi | Ujerumani | Ureno | Uswidi |
![]() |
Makala hii kuhusu maeneo ya Italia bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Italia kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |