Lango:Afrika

Milango ya Wikipedia: Sanaa · Utamaduni · Jiografia · Afya · Historia · Hisabati · Sayansi · Falsafa · Dini · Jamii · Teknolojia

hariri  fuatilia  

Lango la Afrika

Afrika ni bara la pili duniani kwa ukubwa, likiwa na eneo la kilometa za mraba zipatazo 30,370,000 na kwa idadi ya wakazi, hao wakiwa 1,225,080,510 (mwaka 2016). Asia ndiyo bara pekee la kushinda Afrika.

Neno "Afrika" limetokana na lugha ya Kilatini ya Roma ya Kale. Waroma kwa jina hilo hawakumaanisha bara lote bali eneo katika Tunisia ya leo tu. Asili yake ni kabila la "Afrig" lililoishi sehemu zile. Wakati huo Wagiriki wa Kale walitumia zaidi jina la Libya kwa ajili ya nchi kusini kwa Bahari ya Mediteraneo. Maeneo ya ndani kuelekea kusini mara nyingi yaliitwa kwa jina la "Ethiopia" linalomaanisha nchi ya watu weusiweusi (kwa Kigiriki "aithiops": aliyechomwa na jua).

hariri  fuatilia  

Nchi za Afrika

hariri  fuatilia  

Jamii

hariri  fuatilia  

Wasifu Uliochaguliwa

Faili:Hallies.jpg
Haile Selassie wa Ethiopia
Haile Selassie (23 Julai, 189227 Agosti, 1975) alikuwa Kaisari au Negus Negeste wa Ethiopia. Alizaliwa katika kijiji kiitwacho Ejersa. Kabla ya kuwa mfalme aliitwa Ras Tafari Makonnen. Jina lake la kifalme lina maana ya "Utukufu wa Utatu (Mtakatifu)". Pia anafahamika kwa jina la Simba wa Yuda, Mfalme wa wafalme (H.I.M).Baba yake alikuwa mkabaila Mwethiopia aliyeitwa Ras Makonnen akawa gavana wa Harar, familia yake ina watoto 11. Alikuwa Mkristo muumini wa madhehebu ya Orthodoksi ya Ethiopia.


hariri  fuatilia  

Makala iliyochaguliwa

Jameson Hall na Jammie Plaza, mahali spesheli katika kampasi ya juu
Chuo Kikuu cha Cape Town (UCT) ni chuo kikuu cha umma kilicho mjini Cape Town katika jimbo la Rasi ya Magharibi la Afrika Kusini. UCT ilianzishwa mwaka wa 1829 kama South African College, na ndio chuo kikuu kongwe zaidi nchini Afrika Kusini. Kampasi kuu, inayojulikana kama Upper Campus, iko katika Rhodes Estate kwenye mteremko wa Devil's Peak. Kampasi hii ina, katika eneo lililopakiwa kiasi, na vitivo vya Sayansi, Uhandisi, Biashara, na Masomo ya Kibinadamu (isipokuwa idara za sanaa), vilevile Smuts Hall na makazi ya Fuller Hall. Upper Campus imejengwa kuzunguka Jameson Hall, eneo la mahafali na sherehe nyingine, vilevile mitihani mingi. Majengo ya awali na mpangilio wa Upper Campus uliundwa na JM Solomon na kujengwa kati ya 1928 na 1930. Tangu wakati huo, majengo mengi yameongezwa jinsi chuo kimezidi kukua. Upper Campus pia ni nyumbani kwa maktaba kuu iitwayo Chancelor Oppenheimer Library ambayo ina makala mengi ya Chuo Kikuu, kusanyiko la kama milioni 1.3.


hariri  fuatilia  

Picha Iliyochaguliwa


Yasmine Hammamet Medina, Tunisia
(kupata bango)


hariri  fuatilia  

Je, wajua...?

...kwamba Ubuntu au "Obuntu" ni falsafa ya Kiafrika inayosisitiza mahusiano na ushirikiano wa jamii kama msingi wa maisha bora na amani katika jamii. Neno ubuntu limetoka kwenye lugha za Kizulu na KiXhosa za Afrika Kusini. Neno la Kihaya "Obuntu" au kwaKiswahili "utu" linabeba, kwa kiasi fulani, maana ya neno Obuntu.

hariri  fuatilia  

Masharika ya Wikimedia


Nini milango? · Orodha ya Milango